Thursday, 23 April 2015

Maana ya Ujasiriamali

Image result for maana ya ujasiriamaliNini maana ya Ujasiriamali?.

Dhana ya Ujasiriamali ina maana pana , miongoni mwa hizo ni;  Mjasiriamali ni mtu ambaye ana hamasa kubwa ya kuleta mabadiliko chanya  katika hali yake ya kiuchumi ambaye ana tabia za kipekee ili kufanikisha azma yake hiyo kwa kujishuhulisha (yaani kujiajiri) ili awe na hali nzuri zaidi kiuchumi. 


Pia katika hali nyingine   Mjasiriamali  anaweza kuwa mtu yoyote ambaye anajishughulisha mwenyewe(amejiajiri) katika sekta fulani mfano: kilimo, ufugaji au biashara.

Ujasiriamali ni kitendo cha kuwa na tabia ya "Uthubutu". Hii tunaweza kuufananisha na uwezo (fursa) wa kutafuta masoko na kubuni vyanzo vipya vya biashara (Opportunities) ili mradi kuweza kuzalisha mali ama kutoa huduma itakayopelekea kuongeza kipato.

Hata hivyo yote haya yanahitaji muda, fedha na juhudi binafsi (Hii ni sawa na ile dhana inayojulikana kama: "Mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe").


Sifa za Mjasiariamali

Ni mtafutaji Jasiri, anayethubutu kuamua kufanya biashara, mwenye uwezo wa kutambua mapema fursa mbalimbali za biashara, kukabiliana na vikwazo, na kutengeneza faida ya biashara hiyo.
Ujasiriamali ni sawa na usanii ambao ni lazima uingie ucheze sehemu yako mwenyewe. Mara nyingi bila kuwapo usimamizi wa biashara na uwepo wako unaweza kupoteza mwelekeo.

No comments:

Post a Comment