Friday, 24 April 2015

Jinsi ya kupata mtaji

Nini maana ya mtaji?
Watu wengi wanaufahamu "Mtaji"  kwa lugha rahisi kama "Kianzio" cha biashara. Ni kweli, kwa mfano mtaji wa mama Ntilie ni Maji, sufuria, jiko, mkaa, mwiko, sahani, pamoja na fedha ya kununulia chakula kama mchele, nyanya, maharage, chumvi n.k.
Sasa basi katika mtiririko wa mahitaji yaliyotajwa hapo, vyote vinahitaji pesa ili kuvipata.

  1. Kukopa toka Benki au Mashirika ya Mikopo
Benki ni sehemu moja kubwa kabisa ambayo unaweza kuitumia kuipata fedha za mtaji. Watu wenye fedha wanaweka fedha zao hapo kwa ajili ya usalama. Benki wanatumia fedha hizo kuzalisha zaidi kwakuwekeza katika sehemu mbalimbali ikiwemo kutoa mikopo kwa biashara zenye uwezo wa kurudisha kwa faida.

Unachotakiwa kuwaonesha benki ni kuwa unabishara yenye mpango mzuri na unaweza kurudisha fedha hiyo ikiwemo riba ambayo ni faida yao.

Unaweza ukaanza na kiasi kidogo tu kama Milioni 1-5 na ukiweza kurudisha kama inavyotakikana basi unakuwa umejenga uaminifu na hivyo kuwa rahisi unapoomba kwa mara nyingine.

Ukiwa katika kikundi klwabaadhi ya mashrikaya fedha ni rahisi zaidi kupata mkopo kuliko ukiwa peke yako.Ukiwa na mali kama ardhi,nyumba au hata gari unaongeza uwezekano wa kuaminika na kupewa mkopo.

2.  Vikundi vya Kuweka na Kukopa na Vikoba
Vikundi vya kuweka na kukopa na vile vya kuchangiana kwa madhumuni ya kukusanya fedha nyingi ya kutosha kufanya jambo kubwa kwa mmoja wa wanakikundi ni jinsi mojawapo ya kutumia fedha za watu wengine kujiendeleza.
Tengeneza mpango wa biashara ambao una faida na chukua fedha katika kikundi chako ulichojisajili. Hakikisha bishara yako inaweza kurudisha fedha kwa wakati kulingana na masharti ya kikundi chenu.


3. Kukopa toka Kwa Ndugu na Marafiki
Ndugu zako au marafiki ni mojawapo ya sehemu ya kupata mkopo. Mara nyingi mikopo ya watu hawa haina masharti magumu sana,japo ni hatari kama utashindwa kurudishakama ilivyopangwa kwani utahatarisha uhusiano wako nao.

Wakati mmoja katika familia ni masikini au anakosa mtaji wa bishara kuna ndugu mwingine anafedha isiyotumika kukua na kuleta faida (Fedha iliyolala). Tafuta jinsi ya kushawishi fedha hii itumike kujizalisha na mazao ya mtaji huo uwafaidishe wote,wewe mkopaji na mwenye fedha.

Uaminifu ni kitu cha msingi sana katika kufanikisha hili. Ukiwa mtu unayeaminika ni rahisi kwa ndugu na marafiki kukuamini na fedha zao. Uaminifu
ni mtaji mkubwa katika mchezo wa fedha.

No comments:

Post a Comment